Usilie tena, Mama anajua
Futa
machozi, utabasamu kama maua
Furaha
yako, uchungu wako, yote anafahamu
Usikate
tamaa, hata kama moyo umejawa na ugumu.
Jipe
moyo, maisha ni zaidi ya maonyesho
Usikate
tamaa leo, kwa faida ya kesho
Kaza
mshipi, weka malengo
Na
Mama anajua, maisha yana wapi pengo.
Mwiba
moyoni
Uchungu
akilini
Macho
yanavimba; Kwa nini haya yote?
Usilie,
tulia, Bikira Maria anajua yote.
Hata
kama mwilini baridi kali
Tazama
furaha inaguruma, haipo mbali
Ili
ombi hewani ni unyenyekevu
Tukae
na kusali bila uvivu.
Basi,
tabasamu kidogo
Ili
moyo uepuke kuishi na mzigo
Kwa
kuwa maisha ni baraka si adhabu
Iliyopangwa
na Mungu kuendeshwa kwa utaratibu.
Sasa
simama ucheze ngoma ya heshima kwa furaha
Bila
kujali maisha ya kisasa
Na
bila kutembea na kucheza kwa hofu
Kwa
kuwa furaha pekee, daima yaponya miguu mibovu.
