Saturday, 27 November 2021

NI UKOMA KABISA na Joseph C. Ogbu (JoeNwaOgbu)

Wapi unaogelea huu ukoma wangu
Kwako nakimbilia ee Mungu wangu,
Magoti chini; macho kwako
Tutazame usoni; Sisi watoto wako.

Sauti nzuri tena katulisha kwetu sasa,
Lo! kila tabia mbaya, ukoma kabisa
Tuziache na tufuate mazuri kwa unyenyekevu
Ili daima tuishi kwa furaha na utulivu.

Uendelee kukaa nasi ee Mungu Mwema
Wala usisite kutuponya katika kila wetu ukoma
Tuweze tena kukuimbia nyimbo zetu nzuri
Kwa kututendea haya makubwa mazuri.

Ee Mungu Mwenyezi wa milele
Naomba uendelee kutuongoza mbele,
Utuponye jumla bila kubakiza hata kipengele
Maisha yetu yapambwe na amani na vigelegele
Ili nyumba zetu; mfano mzuri huku na kule
Na njia zetu; mafanikio na baraka tele.


…...…..................................................................
....................................................
Wazo lililotengenezwa kutoka kwa maneno ya Baba Abate Pambo Martin Mkorwe OSB,  "KWA HUSU UKOMA" ~ 26/11/2021

Friday, 12 November 2021

KUMBE NDO KINACHOENDELEA NYUMBANI na Joseph C. Ogbu (JoeNwaOgbu)

Habari njema imetufikia; Watanzania furahini
Mapadre,watawa, walei, sote simameni
Tutazame tulikotokea, tulipo na tunapoelekea 
Kweli, furaha kubwa kwetu Tanzania.

Sinodi ya Maaskofu; Mkutano Mkuu wa Mababa
Kaitisha yule Mkuu, Francis wetu Papa
Imani yetu idumu, mpaka tufike kwa Baba
Liishi Kanisa letu, lisafiri bila kusimama.

Kumbe ndo kinachoendelea katika Kanisa
Nasi tuko imara kushiriki kabisa
Tutembee pamoja sote katika umoja
Tusiache fuatilia, kila hatua-na-hoja.

Kwa pamoja na ushirikiano tutaweza
Katika umoja tutafurahi na kucheza
Sinodi hii, ya ulimwengu wote
Njooni haraka tutembee pamoja sote.

Mashaka ondoeni, wasiwasi fukuza
Pamoja tusafiri, sikubali kuachwa
Nyuma we sibaki, tukalijenge Kanisa
Umoja Sinodi, uwazi, ukweli kila hatua.

Kina baba na mama, furahini
Amka wewe kijana, watoto msibaki
Amkeni mliolala, mbiu yapigwa Sinodi
Si ndoto tena, sinodi i mlangoni.

Wako mchango muhimu, msaadao hakika
Uthamini ee ndugu, dumisha ushirika
Kwa nini usishiriki? Sipishane na baraka
Tumikia Kanisa hili, na thawabu tapata
 
Majimbo yote, njooni mchote baraka
Msisite, msichelewe kabisa; kimbieni haraka 
Mama Kanisa anayofuraha kusema; karibuni
Na msiogope Kupiga hodi nyumbani.

Wapendwa, tusikilizeni utaratibu wa majimbo yetu
Tuweze kulisaidia Kanisa kwa utaalamu wetu
Kwa unyenyekevu na upendo wa dhati
Ili tuendelee kufurahia ulimwengu kama Umati.

(Sinodi ya XVI ya Maaskofu  kiulimwengu 2021-2023)



Wednesday, 29 September 2021

HEKIMA YA BABA; IDUMU MILELE na Joseph C. Ogbu (JoeNwaOgbu) 28-09-2021

Bora uchukiwe sababu ya wivu
Utokanao na wako mfano bora 
Si kwa sababu kutokujitahidi na uvivu 
Au kuchukia kazi na kulala kila mara.

Simama, vaa mkanda; acha kushika mashavu
Usiogope, kila siku inatujia na yake nguvu
Maisha mazuri sana, kabisa si mabovu
Kazi hazikwepeki; mweke Mungu mbele, bila  ulegevu.

Hekima ya Baba iendelee kudumu milele
Inasikika masikioni bila hata kelele 
Na hu i pa miguu nguvu kusonga mbele 
Na daima huua maovu kama mshale.

…...…..................................................................
....................................................
Wazo lililotengenezwa kutoka kwa maneno ya Baba Askofu Mkuu Geravas M.  Nyaisonga,
28/09/2021

Friday, 17 September 2021

LADY AFRICA; WE SING THY PRAISE by Joseph C. Ogbu (JoeNwaOgbu)

Smart land, beautiful home
Painted with a purified colour
Dazzling even in the darkest part,
Like Smart damsel, like beautiful star
Your image, our replica
Devoid of any cosmetic colouration
Pure as gold unrefined!
Like queen on a throne; oh beautiful Creature
Vibrant voice always; elegant!
We are the true seeds
That bear the virtues with which thou are made,
Thou are the breast that feeds all,
And "We", the offspring that sing thy praise!

Arise Africans! Let us jubilate
Our home, immaculate; let us celebrate,
Yes! Africa; a beautiful family to desire,
A Mother, who remains not to retire,
Good heart, her nature!
Indiscrimination, her culture!
Love cum unison, her song,
And equity; ever sounds her gong,
Calling children not to ruin Mother’s integrity
Even when wind seems blowing beyond their capacity,
Remember, With God, we shall live to hold our angelic culture,
For the sake of present harmony, and for the future.

I love Thee Mother Africa
We love Thee, Lady Africa.

Friday, 25 June 2021

FRIENDSHIP IN BROTHERHOOD by Joseph C. Ogbu(JoeNwaOgbu)

God, joyously brought us together
And kept us fit and firm in every weather,
To gladly  live as friends and Brothers
Though born of different Fathers,
Arrived to embark on a single mission
To give light and life  to a divinely vision.

Yes! Like unbreakable cord we shall remain
Our  unity we shall ever keep and maintain,
With joy, we must sing a victorious song
With God, we shall move  and remain strong,
Thank You Lord for the gift of fraternal oneness
Which flows from Your incomparable holiness.

Brothers; Let's not forget but our true Love
No matter where life may move us to live,
Let our joy and good hearts not grab an end here
But should be truly given to people living  everywhere,
And let distances of our dioceses be not a barrier
To visit every Brother evangelizing in a particular area.

Brothers; Though Kipalapala, 2021 we departed
But know that, our brotherhood can never be separated,
Though eyes will definitely miss  brothers faces
But heart will surely remember all, in your various bases,
No matter where one may be working or evangelizing
Don't worry; Friendship will keep blossoming and not fading.

Brothers, Wherever we go;  let's keep remembering Mpanda
Arusha, Mbinga, Kayanga, and Bunda,
Moshi, Geita,  Mbeya, and Tabora 
 Morogoro , Shinyanga and  Rulenge-Ngara, 
Dar-es-Salaam, Mahenge and Kahama
Bukoba, Ifakara, Mwanza and Kigoma.

Then, nothing more I have but to wish  everyone well
May our lives be filled with good luck and nice stories to tell,
May God bless our paths and make us true Ministers
So that people may gladly sing to testify our good characters,
Then, with a humble heart  I pray; Lord please always hold us tight
And daily lead us on every road that is right.

Thursday, 3 June 2021

KIPALAPALA MAMA MZAZI, MAMA MLEZI na Joseph C. Ogbu (JoeNwaOgbu)

Shukrani kwako, Mama mzazi
Mambo yako yanaonekana waziwazi
Umetusafisha na kutuvalisha mavazi
Umetulea na kutufundisha Kazi
Nyumbani Kipalapala, mazuri makazi
Twakushukuru Mama; daima tunasema asante.

Kulea watoto, Mama kweli unaweza
Wimbo mzuri miguuni umetuachia  kucheza
Maisha yetu bora, kweli  umeyatengeneza
Upendo; Mama umetupatia bila kubakiza
Huu wosia, basi tuende kuutekeleza
Twakushukuru Mama; daima tunasema asante.

Mengi mazuri, kwako tumepata
Njia yako, tunakiri inameremeta
Malezi Safi, mengi tumechota
Tumeishi kweli, bila kujuta
Asante Mungu; Kip umetuleta
Twakushukuru Mama; daima tunasema asante.

Mama basi kwakheri! Tutarudi kukusalimia
Baraka zako; tunajua popote zitatufikia
Baki salama; Imani uendelee kuipalilia
Usiku na mchana, nguvu umetutia
Asante Sana, kutuonyesha hii njia
Twakushukuru Mama; daima tunasema asante.

Basi kwakheri, Mama Kipalapala
Tunakupenda sana, bila  hila
Mama asante, umetupatia fadhila
Ukarimu wako, hauna mjadala
Kwakheri Mama, umetusaidia jumla
Twakushukuru Mama; daima tunasema asanteee.

Wednesday, 14 April 2021

Loo! TAZAMENI MWANAMKE MZURI SANA na Joseph C. Ogbu (JoeNwaOgbu)


SHANGWE SHANGWE KWAKO; EE MTAKATIFU YOSEFU na Joseph C. Ogbu (JoeNwaOgbu)

Ee Mtakatifu wetu Yosefu; Kwa unyenyekevu mkubwa  twakusifu,
Daima unastahili nyimbo zetu; Pamoja na parapanda zetu,
Duniani kote furahini pamoja; Tusherekee mwaka katika umoja,
Kwa shangwe na vigelegele; Kumshangilia hapa na pale,
Mtakatifu wetu, Baba Yetu; Msimamizi wetu, Mlinzi wetu,
Huu ndo mwaka wako; Tunaomba Mtakatifu Yosefu, Utuombee.

Kanisa linajivunia sana Baba; Sababu hutembea nawe sambamba,
Ulimwenguni kote  wakufurahia daima; Kwa sababu  ya wako wema,
Mtakatifu mwenye imani thabiti; Kwa Mungu bila kumsaliti,
Kwa upole, kamchukua Maria; Bila kumdharau au kumchukia, 
Mume wa Maria Bikira; Daima twakuimbia kwa furaha,
Huu ndo mwaka wako; Tunaomba Mtakatifu Yosefu, Utuombee.

Mtakatifu Yosefu Baba mwema; Mwenye unyenyekevu na huruma,
Baba mlishi wa Yesu; Mwaka huu rasmi unakuhusu,
Umahiri wako ni wa ajabu; Kumbe ndo kwetu sababu,
Kukusherekea kabisa huu mwaka; Kwa utaratibu bila haraka,
Ujasiri wako hauna mfano; Unasifiwa katika kila mkutano,
Huu ndo mwaka wako; Tunaomba Mtakatifu Yosefu, Utuombee.

Yosefu mpole  na  msikivu; Kazi umefanya bila uchovu,
Sote unatulinda hapa ulimwenguni; Ili tusijikute kule mavumbini
Mwombezi wa wenye shida; Yote hufanya kwa kiada,
Msimamizi wa wafanyakazi; Njia yako si  hasi,
Dunia nzima Baba inakutegemea; Ukweli tunajua nasi unatuombea,
Huu ndo mwaka wako; Tunaomba Mtakatifu Yosefu, Utuombee.

Basi Baba yetu Mtakatifu; Sisi Watoto wako wakosefu,
Twakuomba utufundishe wako Ukarimu; Tutembee  katika misingi muhimu,
Mtakatifu wetu Mwenye haki; Utuombee kwa Mungu atubariki,
Tuwe  daima na upendo; pasipo kuwa na makandokando
Na utuombee kifo chema; Tuweze kumwona Mungu Mwema, 
Huu ndo mwaka wako; Tunaomba Mtakatifu Yosefu, Utuombee.

SMILE ON THE FACE; BUT...? by Fr. Joseph C. Ogbu

Imagine! Calmly water turning thicker than blood, Evils gently overflowing like flood. God! be merciful on your precious world, And allow n...