Monday, 8 June 2020

MIMI MTAJIRI na Joseph C. Ogbu (JoeNwaOgbu)

Yangu ni kukushukuru; Na wala si  kukufuru,
Magoti  chini nakuomba; Baba tusafiri sambamba,
Mkono wako wa nguvu; hakika huponya maumivu,
Naomba niseme asante;  bila Wewe dunia haifai lolote,
Asante Baba kwa maisha; mengi bora menihifadhia kwa bahasha,
Nyumba hata sina kabisa; na sielewi wapi nipate tena hisa,
Lakini utajiri hushuka kama umande; kwa kuwa Baba haangalii upande,
Loo! Kumbe  mimi ni tajiri sana;  basi kamwe Baba sitakutukana,
Siku zote  furaha moyoni;  amani rohoni na afya mwilini,
 Haya yote kabisa  si haba; nasema asante ee Wangu  Baba,
Kwa kuwa  umenifanya mtajiri; hata kama pesa imegoma kuja alfajiri,
Asante sana Baba Yangu; kwa zawadi yako mlangoni mwangu,
Basi tusimame wote wadau; tuchezecheze bila  kusahau;
Kujitunza katika upendo na amani; ndo  utajiri wa kwanza maishani,
Daima mikono itaelekea  juu; kukushukuru Wewe uliye na Ukuu,
Kwa kufanya ulimi kuonja huu utajiri; kwa kuwa huo ndio safi ujasiri,
Lakini daima sitamsahau Mama Mpenzi; Bikira Maria, Mama Safi Sana,
Mwombezi wangu; mahitaji yangu, yote kayafikisha kwa Mungu, 
Asante Sana Mama, Mimi na Wewe daima.

SMILE ON THE FACE; BUT...? by Fr. Joseph C. Ogbu

Imagine! Calmly water turning thicker than blood, Evils gently overflowing like flood. God! be merciful on your precious world, And allow n...