Wednesday, 29 September 2021

HEKIMA YA BABA; IDUMU MILELE na Joseph C. Ogbu (JoeNwaOgbu) 28-09-2021

Bora uchukiwe sababu ya wivu
Utokanao na wako mfano bora 
Si kwa sababu kutokujitahidi na uvivu 
Au kuchukia kazi na kulala kila mara.

Simama, vaa mkanda; acha kushika mashavu
Usiogope, kila siku inatujia na yake nguvu
Maisha mazuri sana, kabisa si mabovu
Kazi hazikwepeki; mweke Mungu mbele, bila  ulegevu.

Hekima ya Baba iendelee kudumu milele
Inasikika masikioni bila hata kelele 
Na hu i pa miguu nguvu kusonga mbele 
Na daima huua maovu kama mshale.

…...…..................................................................
....................................................
Wazo lililotengenezwa kutoka kwa maneno ya Baba Askofu Mkuu Geravas M.  Nyaisonga,
28/09/2021

6 comments:

  1. Hakika idumu na kudumu,
    Isipite bila ya umuhimu,
    Wa leo umuhimu kesho hukumu,
    Dhamiri kipimo cha ukweli mgumu!

    ReplyDelete
  2. Utunzi bora timamu,kongole kwako baba,
    Kiswahili mehitimu, wakijulia si haba,
    Ukawe mwema mwalimu,katapike uloshiba,
    Hongera ogbu hongera, kipaji chako ni lulu.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Bila kuwa na haraka, naomba niseme asante Kaka, na Mungu Mwenyezi awakinge na awajalie baraka.

      Delete
  3. Olomi wangu mkono, twende tukampongeze,
    Utari uso kikomo, karama aendeleze,
    Havitukifu vigano, vya Radha bila ya zeze,
    Ogbu zako kongore, zidi kutupa nasaha

    ReplyDelete
    Replies
    1. Hahaha, mwalimuu tayari kaandika, wanafunzi sasa tutulie; hakuna namna, kuelewa ngumu, basi tusilie; misamiati migumu,anakuja kutuelezea, hahaha tuvumilie. Shukrani Sana Baba kwa comment yako!!! Pamoja Sana Baba.

      Delete

SMILE ON THE FACE; BUT...? by Fr. Joseph C. Ogbu

Imagine! Calmly water turning thicker than blood, Evils gently overflowing like flood. God! be merciful on your precious world, And allow n...