Monday, 6 July 2020

JoenwaOgbu

BADO IPO, HAIJAPOTEA na Joseph C. Ogbu (JoenwaOgbu)

Naomba toa mkono kidevuni
Na ufute machozi mashavuni,
Nini haki yako unawaza imepotea
Muamini Mungu tu atakurudishia,
Maisha haya ndo kawaida yake
Ni kama fumbo maanayake,
Acha kufadhaika, ni muda wa kutabasamu
Furahi! Mungu hatakuacha kwenye jamu,
Basi simama, Mama anakuita! Toka kwenye mahangaiko yako
Na ujue daima, Mama na Mwanaye hawataacha kuwa Wasaidizi wako.

Friday, 3 July 2020

ETI,VIJANA LEO SIYO YENU NGOJENI KESHO! na John K. Semindu



Eti,vijana leo siyo yenu ngojeni kesho! Hahahaha... Msemo huu hauna tofauti na ule usemao “Vijana ni taifa la kesho”! Mnanitia uvivu kutumia nguvu, akili na vipaji vyangu kufanikisha mambo kwa kuingojea kesho yenu isiyofika. Hivi kesho ilishawahikufika? Na ikishafika Inaitwaje? Ikikaribia haiitwi tena kesho hiyo ni leo, ndiyo sasa. Na siku ile uliyoitumia kusema kesho itaitwa jana. Kesho iko wapi? …haaaaaa!.. ndiyo ile imeitwa jana au ndiyo hii inaitwa leo? Wewe kesho, mbona hufiki? Kumbe jana ni halisi na leo pia ni halisi kwamaana jana imepita na leo ndiyo sasa, lakini kesho haijafika. Hakika kesho haijawahi fika, kesho haijawahi kuwa, inabaki akilini tu. Kesho uniache, mimi najituma sasa.

Utasikia mmoja anasema, ndugu yangu nivumilie kidogo kesho nitakupatia mzigo wako; na mwingine anasema, rafiki kesho nitakutumia pesa kidogo. Hizi ni baadhi ya kauli za kuleta matumaini kuifikia kesho japo haifikiki. Atakapokupatia mzigo wako siyo tena kesho bali ni leo;  akikutumia pesa siyo tena kesho bali ni sasa. Kesho itaendelea kubaki kwenye akili na siyo kwenye uhalisia.                                    Nifupishe tu maneno, kwamba kesho haifiki daima. Hata uwe na mbio kiasi gani huwezi kuifikia kesho, na hata uwe mrefu wa futi nane kama Robert Wadlow huwezi kuiona kesho. Labda wanasayansi watusaidie ndege za mwendokasi tuikimbize; wenzenu wa Dar-essalaam wana mabasi ya mwendo kasi lakini mpaka sasa bado hawajaifikia kesho. Labda Flyovers zitawapa matumaini ya kuifikia kesho.

Falsafa hii ya maisha (vijana taifa la kesho) inanyima fursa na kudogosha vijana katika bidii za kuleta maendeleo katika jamii. Kauli hii hufubaisha fikra kwa vijana na kupelekea vijana kungojea kupewa amri na kufanyiwa vitu vingi bila wao kushiriki kikamilifu au kujituma kikamilifu kwa maana leo siyo yao wanangoja kesho ambayo haijawahi kufika.

Kauli hii inatoa fursa zaidi kwa wale walio vuka umri wa ujana (watu wazima) kuwadharauna kuwadogosha vijana katika kutoa mawazo, mapendekezo na hata kusimamia misimamo yao katika maisha ya kila siku. Nazani ulishawahi kusikia au kuambiwa “utatuambia nini? Wewe bado kijana sana, subiri ukue ndiyo utoe mawazo, tusikilize sisi wazee kwanza”. Sitaki kukwambia usiwasikilize wazee bali ninyi mlio wazee wapeni vijana nafasi ya kutoa mawazo bila kuwabeza kwa kauli za namna hiyo maana vijana wana fikra motomoto. Ndiyo kusema kwamba, malumbano mengi na misuguano hasi ya kimawazo kati ya vijana na watu wazima huanzia kwenye falsafa hii ya vijana taifa la kesho au kusema vijana leo siyo yenu ngojeni kesho.

Mimi niliye kijana ninayesukumwa na moyo wangu kuhitaji usalama, uhuru, kufaulu, utulivu moyoni na kupata heshima ndiye taifa la sasa, leo ndiyo yangu kwa maana natambua kwamba kesho haijawahi kufika na hata ikifika siyo tena kesho na ikipita siyo tena kesho. Vijana muda ni sasa tusingoje kesho...! Tusipumbazwe na kauli "vijana taifa la kesho" hii itafaa kwa watoto. Nasema tena, achana na falsafa ya ngoja kesho wewe ni taifa la sasa.
Vijana leo ndiyo yetu, kesho haifiki.

Sunday, 28 June 2020

SWEETHEART IS VIRGIN by Joseph C. Ogbu (JoenwaOgbu)


 Permit me to explode my love
Forget my weaknesses for you I have
Before your hut, I stand to dance
Open your door, a word I have to pronounce
Listen to my poor voice, I have something to sing
 Pay heed to my plea, that my life may not develop a wing
 Oh Sweetheart, please reject not my love
For my heart, Love; I ever stay to give
My Love! It's You; I will daily love with no tarry
You are Virgin, You are Blessed and Mother, You are Mary
Then, Beloved Mom, teach me how to love faithfully
Even when its reward may be painful and seem ugly.

Monday, 8 June 2020

MIMI MTAJIRI na Joseph C. Ogbu (JoeNwaOgbu)

Yangu ni kukushukuru; Na wala si  kukufuru,
Magoti  chini nakuomba; Baba tusafiri sambamba,
Mkono wako wa nguvu; hakika huponya maumivu,
Naomba niseme asante;  bila Wewe dunia haifai lolote,
Asante Baba kwa maisha; mengi bora menihifadhia kwa bahasha,
Nyumba hata sina kabisa; na sielewi wapi nipate tena hisa,
Lakini utajiri hushuka kama umande; kwa kuwa Baba haangalii upande,
Loo! Kumbe  mimi ni tajiri sana;  basi kamwe Baba sitakutukana,
Siku zote  furaha moyoni;  amani rohoni na afya mwilini,
 Haya yote kabisa  si haba; nasema asante ee Wangu  Baba,
Kwa kuwa  umenifanya mtajiri; hata kama pesa imegoma kuja alfajiri,
Asante sana Baba Yangu; kwa zawadi yako mlangoni mwangu,
Basi tusimame wote wadau; tuchezecheze bila  kusahau;
Kujitunza katika upendo na amani; ndo  utajiri wa kwanza maishani,
Daima mikono itaelekea  juu; kukushukuru Wewe uliye na Ukuu,
Kwa kufanya ulimi kuonja huu utajiri; kwa kuwa huo ndio safi ujasiri,
Lakini daima sitamsahau Mama Mpenzi; Bikira Maria, Mama Safi Sana,
Mwombezi wangu; mahitaji yangu, yote kayafikisha kwa Mungu, 
Asante Sana Mama, Mimi na Wewe daima.

Sunday, 24 May 2020

IENDELEE KUMEREMETA na Joseph C. Ogbu(JoeNwaOgbu)

Peke yako, sitakuacha
Wewe upendo, sitakuficha.
Upendo hujenga maisha yawe imara,
Kabisa kupenda haina hasara.
Nashangaa tena hauna hata tabaka,
Ila ndani hujazwa tupu baraka.
Loo! zawadi kubwa sana tulizojaliwa,
Kugawia wenye nguvu na waliolemewa;
Sawa kwa wakubwa na pia kwa wadogo.
Tukijua upendo una nguvu si kidogo;
Basi Upendo mikononi tushike sote,
Ili dunia iendelee kumeremeta kwa wote.

Monday, 4 May 2020

Eee MPENZI WANGU na Joseph C. Ogbu (JoeNwaOgbu)


  Unishike Mpenzi wangu nifurahi; Kukaa Nawe kabisa si mwiko
Midomo yangu tu Shukrani; Nikumbukapo Uzuri Wako,
Moyo wangu unashangilia; Wema Wako nafaidia
Uwepo Wako nafurahia; Huruma Yako yasaidia,
Kwa moyo safi nasherekea; Sura Yako nasemea
 Wimbo wangu nimekuletea; Ngoma safi imekolea,
 Hapa sasa unifundishe;  Kukuweka mbele katika kila jambo
Kwa Neno Lako wala sibishe;  Kwa kuwa Wewe ujuaye yote mambo,
Pamoja Nawe ni kwangu bahati; Kukaa Nawe ijaayo maisha amani
Uniongoze nikufuate kwa moyo dhati;  Hapa sasa na pote mahalini,
Na Uujaze moyo kwa upendo; Ili moyo daima ukose nafasi ya chuki
Najua njia Yako haina magendo; Na neema Zako zinalinda miguu katika dhiki,
Basi Eee Mungu Wangu; Uniongoze katika njia zako
Ili nitimize ulichoweka kwangu; Na mwisho nije salama Kwako.

SMILE ON THE FACE; BUT...? by Fr. Joseph C. Ogbu

Imagine! Calmly water turning thicker than blood, Evils gently overflowing like flood. God! be merciful on your precious world, And allow n...