Wednesday, 8 July 2020
Monday, 6 July 2020
BADO IPO, HAIJAPOTEA na Joseph C. Ogbu (JoenwaOgbu)
Naomba
toa mkono kidevuni
Na
ufute machozi mashavuni,
Nini
haki yako unawaza imepotea
Muamini
Mungu tu atakurudishia,
Maisha
haya ndo kawaida yake
Ni
kama fumbo maanayake,
Acha
kufadhaika, ni muda wa kutabasamu
Furahi!
Mungu hatakuacha kwenye jamu,
Basi
simama, Mama anakuita! Toka kwenye mahangaiko yako
Na
ujue daima, Mama na Mwanaye hawataacha kuwa Wasaidizi wako.
Friday, 3 July 2020
ETI,VIJANA LEO SIYO YENU NGOJENI KESHO! na John K. Semindu
Eti,vijana leo siyo yenu ngojeni kesho! Hahahaha...
Msemo huu hauna tofauti na ule usemao “Vijana ni taifa la kesho”! Mnanitia uvivu
kutumia nguvu, akili na vipaji vyangu kufanikisha mambo kwa kuingojea kesho yenu
isiyofika. Hivi kesho ilishawahikufika? Na ikishafika Inaitwaje? Ikikaribia
haiitwi tena kesho hiyo ni leo, ndiyo sasa. Na siku ile uliyoitumia kusema
kesho itaitwa jana. Kesho iko wapi? …haaaaaa!.. ndiyo ile imeitwa jana au ndiyo
hii inaitwa leo? Wewe kesho, mbona hufiki? Kumbe jana ni halisi na leo pia ni halisi
kwamaana jana imepita na leo ndiyo sasa, lakini kesho haijafika. Hakika kesho haijawahi
fika, kesho haijawahi kuwa, inabaki akilini tu. Kesho uniache, mimi najituma sasa.
Utasikia mmoja anasema, ndugu yangu nivumilie kidogo
kesho nitakupatia mzigo wako; na mwingine anasema, rafiki kesho nitakutumia pesa
kidogo. Hizi ni baadhi ya kauli za kuleta matumaini kuifikia kesho japo haifikiki.
Atakapokupatia mzigo wako siyo tena kesho bali ni leo; akikutumia pesa siyo tena kesho bali ni sasa.
Kesho itaendelea kubaki kwenye akili na siyo kwenye uhalisia. Nifupishe tu maneno, kwamba
kesho haifiki daima. Hata uwe na mbio kiasi gani huwezi kuifikia kesho, na hata
uwe mrefu wa futi nane kama Robert Wadlow huwezi kuiona kesho. Labda wanasayansi
watusaidie ndege za mwendokasi tuikimbize; wenzenu wa Dar-essalaam wana mabasi ya
mwendo kasi lakini mpaka sasa bado hawajaifikia kesho. Labda Flyovers zitawapa matumaini
ya kuifikia kesho.
Falsafa hii ya maisha (vijana taifa la kesho) inanyima
fursa na kudogosha vijana katika bidii za kuleta maendeleo katika jamii. Kauli hii
hufubaisha fikra kwa vijana na kupelekea vijana kungojea kupewa amri na kufanyiwa
vitu vingi bila wao kushiriki kikamilifu au kujituma kikamilifu kwa maana leo siyo
yao wanangoja kesho ambayo haijawahi kufika.
Kauli hii inatoa fursa zaidi kwa wale walio vuka umri
wa ujana (watu wazima) kuwadharauna kuwadogosha vijana katika kutoa mawazo, mapendekezo
na hata kusimamia misimamo yao katika maisha ya kila siku. Nazani ulishawahi kusikia
au kuambiwa “utatuambia nini? Wewe bado kijana sana, subiri ukue ndiyo utoe mawazo,
tusikilize sisi wazee kwanza”. Sitaki kukwambia usiwasikilize wazee bali ninyi mlio
wazee wapeni vijana nafasi ya kutoa mawazo bila kuwabeza kwa kauli za namna hiyo
maana vijana wana fikra motomoto. Ndiyo kusema kwamba, malumbano mengi na misuguano
hasi ya kimawazo kati ya vijana na watu wazima huanzia kwenye falsafa hii ya vijana
taifa la kesho au kusema vijana leo siyo yenu ngojeni kesho.
Mimi niliye kijana ninayesukumwa na moyo wangu kuhitaji
usalama, uhuru, kufaulu, utulivu moyoni na kupata heshima ndiye taifa la sasa, leo
ndiyo yangu kwa maana natambua kwamba kesho haijawahi kufika na hata ikifika siyo
tena kesho na ikipita siyo tena kesho. Vijana muda ni sasa tusingoje kesho...! Tusipumbazwe
na kauli "vijana taifa la kesho" hii itafaa kwa watoto. Nasema tena, achana
na falsafa ya ngoja kesho wewe ni taifa la sasa.
Vijana
leo ndiyo yetu, kesho haifiki.
Sunday, 28 June 2020
SWEETHEART IS VIRGIN by Joseph C. Ogbu (JoenwaOgbu)
Permit me to explode my love
Forget my weaknesses for you I have
Before your hut, I stand to
dance
Open your door, a word I have
to pronounce
Listen to my poor voice, I have
something to sing
Pay heed to my plea, that my life may not develop
a wing
Oh Sweetheart, please reject not my love
For my heart, Love; I ever stay to give
My Love! It's You; I will daily
love with no tarry
You are Virgin, You are Blessed
and Mother, You are Mary
Then, Beloved Mom, teach me how to
love faithfully
Even when its reward may be
painful and seem ugly.
Monday, 8 June 2020
MIMI MTAJIRI na Joseph C. Ogbu (JoeNwaOgbu)
Yangu
ni kukushukuru; Na wala si kukufuru,
Magoti
chini nakuomba; Baba tusafiri sambamba,
Mkono
wako wa nguvu; hakika huponya maumivu,
Naomba
niseme asante; bila Wewe dunia haifai
lolote,
Asante
Baba kwa maisha; mengi bora menihifadhia kwa bahasha,
Nyumba
hata sina kabisa; na sielewi wapi nipate tena hisa,
Lakini
utajiri hushuka kama umande; kwa kuwa Baba haangalii upande,
Loo!
Kumbe mimi ni tajiri sana; basi kamwe Baba sitakutukana,
Siku
zote furaha moyoni; amani rohoni na afya mwilini,
Haya yote kabisa si haba; nasema asante ee Wangu Baba,
Kwa
kuwa umenifanya mtajiri; hata kama pesa imegoma
kuja alfajiri,
Asante
sana Baba Yangu; kwa zawadi yako mlangoni mwangu,
Basi
tusimame wote wadau; tuchezecheze bila kusahau;
Kujitunza
katika upendo na amani; ndo utajiri wa
kwanza maishani,
Daima
mikono itaelekea juu; kukushukuru Wewe
uliye na Ukuu,
Kwa
kufanya ulimi kuonja huu utajiri; kwa kuwa huo ndio safi ujasiri,
Lakini daima sitamsahau Mama Mpenzi; Bikira Maria, Mama Safi Sana,
Mwombezi wangu; mahitaji yangu, yote kayafikisha kwa Mungu,
Asante Sana Mama, Mimi na Wewe daima.
Sunday, 24 May 2020
IENDELEE KUMEREMETA na Joseph C. Ogbu(JoeNwaOgbu)
Peke
yako, sitakuacha
Wewe
upendo, sitakuficha.
Upendo
hujenga maisha yawe imara,
Kabisa
kupenda haina hasara.
Nashangaa
tena hauna hata tabaka,
Ila
ndani hujazwa tupu baraka.
Loo!
zawadi kubwa sana tulizojaliwa,
Kugawia
wenye nguvu na waliolemewa;
Sawa
kwa wakubwa na pia kwa wadogo.
Tukijua
upendo una nguvu si kidogo;
Basi
Upendo mikononi tushike sote,
Ili
dunia iendelee kumeremeta kwa wote.
Monday, 4 May 2020
Eee MPENZI WANGU na Joseph C. Ogbu (JoeNwaOgbu)
Unishike
Mpenzi wangu nifurahi; Kukaa Nawe kabisa si mwiko
Midomo
yangu tu Shukrani; Nikumbukapo Uzuri Wako,
Moyo
wangu unashangilia; Wema Wako nafaidia
Uwepo
Wako nafurahia; Huruma Yako yasaidia,
Kwa
moyo safi nasherekea; Sura Yako nasemea
Wimbo wangu nimekuletea; Ngoma safi imekolea,
Hapa sasa unifundishe; Kukuweka mbele katika kila jambo
Kwa
Neno Lako wala sibishe; Kwa kuwa Wewe ujuaye
yote mambo,
Pamoja
Nawe ni kwangu bahati; Kukaa Nawe ijaayo maisha amani
Uniongoze
nikufuate kwa moyo dhati; Hapa sasa na pote
mahalini,
Na
Uujaze moyo kwa upendo; Ili moyo daima ukose nafasi ya chuki
Najua
njia Yako haina magendo; Na neema Zako zinalinda miguu katika dhiki,
Basi
Eee Mungu Wangu; Uniongoze katika njia zako
Ili
nitimize ulichoweka kwangu; Na mwisho nije salama Kwako.
Subscribe to:
Posts (Atom)
SMILE ON THE FACE; BUT...? by Fr. Joseph C. Ogbu
Imagine! Calmly water turning thicker than blood, Evils gently overflowing like flood. God! be merciful on your precious world, And allow n...





